Saturday, November 18, 2017

MAHITAJI YA MWANAUME: KILA SIKU HAKIKISHA ANAFURAHI


man

MAHITAJI YA MWANAUME
1.     Kutoshelezwa ktk tendo la ndoa – kuambiwa umependeza, nakupenda kunaweza kumtosheleza mwanamke lakini sio mwanaume, yeye anahitaji kushiba tendo la ndoa
2.     Heshima – Mwanaume huyatafsiri matendo yote yanayoonyesha heshima kama upendo au penzi kwake, heshima hapa haijalishi umemzidi mume wako kiwango cha elimu, uwezo wa fedha, fursa au hata kujulikana. Wakati mwanaume anajukumu la kuonyesha penzi kwa mke wake, mwanamke hana budi kuonyesha heshima kwa mumewe.
3.     Mwanamke anayevutia – jiweke safi, jitunze na uvutie ili kumfanya mume wako akutosheke
4.     Kiu ya kuwa na nyumbani kusafi – pamoja na kwamba anaweza asiwe msafi kama wewe lakini ana kiu ya kuona kwake ni kusafi. Anatamani marafiki zake wavutiwe na kwake
5.     Kiu ya kukubaliwa (admiration) – pamoja na madhaifu yake bado anakiu ya wewe kutambua mchango wake na kukubali yote yahusuyo taaluma yake, uwezo wake na mafanikio yake. Heshimu na kubali mchango wake ktk familia

Comment