Saturday, July 21, 2018

SIMULIZI YA KUSISIMUA... Ndoa Yangu Inanitesa part 10 mwisho

Tukiwa sebuleni nilianza kumueleza Getruda. Moyo uliniuma kila nilipo kumbuka aliyonifanyia “Mke wangu kama ingenipasa kusema, nini kinacho ikera nafsi yangu ni kuni dhalilisha ndani ya kadamnasi, sio wafanyakazi wangu wa wageni, wote wanafahamu ulilolifanya, na isitoshe ile ni hotel yangu unadiriki kufanya mapenzi ukitoa kashfa ili kuinufaisha jamii, kumbuka aibu si yangu pekee, ni yetu wote.” 

Sijui ni mkate sikio au nimpe kilema kwenye via vya uzazi ni mchome na moto wa umeme (hita)asiweze kufanya tendo la ndoa maisha?.Ndio itakuwa fundisho,kiherehere kitamuisha”wakati na waza cha kumfanyia, nilikatishwa na sauti.

“Mume wangu kumbuka wewe ndio uliyenitafutia mwanaume wa kuniridhisha kimapenzi, ilinijisikie nina mume, basi kama ni hivyo nami sitaki penzi la mtu mwingine wa nje. Nataka penzi lako nilikubali kwa kukuheshimu. Mwanamke kawaida hatafutiwi mume, anatafuta mwenyewe, hisia zote nilizoweka kama nipo na wewe, iweje useme na kudhalilisha, kama utashindwa leo kesho nataka talaka yangu,asubuhi na mapema, umenielewa?”Getrudaalinisemesha kwa ukali.


“Sio nimekukataza usiwe naye, kinachonikera ni kunidhalilisha na kutoa siri ya unyumba wetu, sina wivu na mapenzi yako.Ninachotaka unihifadhie siri moyoni mwako”niliinamisha kichwa chini kama kobe.

“Mume wangu nakutunzia heshima kuliko mtu yeyote duniani, nashangaa!unapo sema nainfaisha jamii. Kama angekuwa msichana mwingine asinge vumilia hata wiki moja, na washukuru wazazi kunifundisha uvumilivu ndani ya nyumba”Aliendelea kuongea,asijue nina mawazo nini moyoni.

Tukiwa kwenye mazungumzo,nilisikia simu ikiita,nilijipapasa kama ilikuwa simu yangu.Nilipotizama pembeni nilimuona Getruda akitoa simu yake kwenye pochi ndogo ya rangi nyeusi iliyojaa nakishi nyingi.

“Hallo, uko wapi?”Getruda alipokea tu,baada ya kuona jina juu ya kioo cha simu.Niligutuka nikahisi mtu huyo anamfahamu,ndio maana alimuuliza aliko.

“Aaaa..nipo Makutano bar hapa napata moja baridi moja moto.Vipi mume bwege yupo?”

“Yupo anakusalimia”Getruda alisema na kunitupia jicho ,akacheka kidogo na kuendelea, “Utakuja kutusalimia?”Getruda aliongea akiniongoa wasi wasi.

“Ninani huyo unaongea naye?”Nilijikuta nikisema wakati Getruda anaongea na simu.

“Wivu umekuzidi mume wangu.Kila kitu unataka kujua hebu chukua basi uongee naye”Getruda aliibadilikia kwa ghafla,alinyoosha mkono wake akitakakunikabidhi simu.

“Sihitaji kuongea nae,nimekuuliza kwani vibaya?.Nilifikiri ni mama amekupigia simu”

“Hapana.Nirafiki yangu”Kisha akaendelea kuongea nae.

“Samahani kwa usumbufu uliojitokeza.Mume wangu anwivu ilembaya”

“Sasa wivu wanini wakati hayawezi?”Sauti nzito upande wa pli ilisikika ikisema.

“Hata mimi nashangaa!”Getruda alidakia na kuangua kicheko kikubwa.

“Mpenzi sikia…..naomba ufike sasa hivi hapa Makutano bar”

“Mama anaumwa sana!.Ehhe mmempeleka hospitali?”Getruda aliongea maneno hayo akiwa tayari kesha kata simu.Aliendelea kuongea simu ikiwa imekatika ilimradi anipumbaze “Ana umwa na nini hasa?” alitulia sekunde mbili hivi akaendelea, “Ooo! My god .Kuna uwezekana wa kupona?”

alitulia tena sekunde kadhaa hivi, “Sawa.Ninakuja sasa hivi huko”Akajidai kukata simu.

“Vipi mbona jasho linakutoka?.Mama anaumwa na nini?”

Nilimwuliza sekunde chache alipokata simu. “Mama alidondoka ngazi akiingia kanisani”Getruda aliongea kiupole kabisa, akionekana kujizuia kulia.

“Kanisani?”

“Ndio.Na hivi sasa yupo amepelekwa hospitali ya Kcmc kwa matibabu” Safari hii alifura na alifanya kulalamika chini chini.

“Ooo! Pole sana mke wangu.Unaonaje nikaoga tukaenda wote?”

“Utanichelewesha sana”

“Basi siogi tena. Ngoja nivae twende,tena nina siku nyingi sijaenda kumsalimu”Niliongea nikiamka kitini, tayari kwa safari.

“Hapana.Nitakuletea taarifa ya hali yake.Nyumba tutamuachia nani?”

“Hilo halina shida.Nisubiri”

“Sitaki bwana. Wee kila mahali unataka kuongozana na mimi.Nimeshachoka, ngoja niende kisha kesho nikirudi nitakuja kukuchukua kwani hata kupajua hupajui.Unapafahamu pale tulipokuwa tukiishi zamani” Nilisimama kama mlingoti ,nikavuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.Nikatikisa kichwa na kusema “Sawa.Kama hutaki nikapajua kwenu leo ….hata kesho nitapajua”

Niliona Getruda akitoa tabasamu kubwa ,hakuishia hapo alinifuata nakunibusu shavuni “Mwaaaa”Kisha akaokota kipima joto chake,na kutoka kwa haraka akionekana mwenye wasi wasi mkubwa.Alipofika mlangoni aligeuka na kunitizama kama akinihurumia vile,sikugundua kitu ,nilibaki nimeduwaa.Akanipungia mkono na kusema “Bye bye”Nami nikapunga kono langu zito kigoigoi bila tabasamu.


Getruda alimpigia simu mteja wetu wa kila siku katika usafi,si mwingine bali Jangala. “HalloJangala tafadhali naomba unichukue hapa nyumbani”alisema baada ya simu kupokelewa.

“Sawa.Namshusha abiria hapa mjini nakuja”

“Ok”Alijibu na kukata simu.

Kama kawaida yake Jangala huwa hakaidi na hana tamaa.Aliingia na kusimama mbele ya Getruda binti Kimario.

“Shem vipi.Wapi leo pa kula kuku.Si unaelewa wiki end”Jangala alimtania Getruda.

“Ndio. Wiki end lakini kwangu imenijia vibaya .Nimepata taarifa mama yangu mgonjwa.Naomba unifikishe karibu na Makutano bar nikampe taarifa shangazi yangu.Kisha utaendelea na safari yako.Mimi nitakupigia kama nitakuhitaji tena”Getruda alidanganya.

“Sawa.Riziki ndogo ndogo hizi usininyime shem.Pole sana kwa kuuguliwa na mama yako”

“Nishapoa shem”Alimjibu kiunyonge.Getruda hakuuguliwa wala nini.Alipokuwa akienda ni Makutano bar kukutana na Mzee Jophu Kundy.

Katika mazungumzo yao walijikuta kufika Makutano bar, “Tafadhali nishushe hapa.Kuna uchochoro gari haliwezi kuingia huko.Shilingi ngapi?”

“Elfu nne zinatosha shem”Jangala alisema akimtizama Getruda.

“Punguza shem.Hujui mimi mteja wako?”

“Petroli imepanda bei sana shem. ‘Any way’ nipe tatu unusu”Jangala alisema .

Getruda alimpatia Jangala elfu tatu na mia tano,akashuka garini. “Usihaike shem.Nitafunga mwenyewe mlango.Mteja kwangu ni mtukufu”Jangala alisema baada ya kumuona Getruda anataka kufunga mlango. Getruda alijidai kama anaingia uchochoroni ili Jangala aondoke zake.Alipogeuka aliona gari la Jangala likiishia bali kabisa.Aligeuka na kurudim kuelekea kule Makutano bar.


*****************

Ndani ya makutano bar,alionekana mwanaume wa makamo.Kwa kumtizama ungeweza kukisia anamiaka hamsini ama hamsini na tano.Kichwa chake kilikuwa na mvi za kuhesabika.Uso wake ulisha anza kuwa na makunyanzi ya uzee.Alivaa suti ya kahawia,na viatu vya pembe nne ‘Four angile’.Shingoni alinyonga tai ya bluu iliyozidi kumfanya maridadi.Mkononi alivaa saa ya seiko 5 ya dhahabu.Meza aliyoketi ilijaa vyakula na vinywaji.


Mara kwa mara aliinua mkono wake wa kushoto akitizama muda,alipomaliza aligugubia glasi ya bia mdomoni na kuirudishia glasimezani.Pia muda wa kuiacha pombe ishuke vema tumboni alitupa macho yake lako la kuingilia wateja.Safari hii ilikuwa mara ya kumi kutizama lango hilo,alipohamisha macho aliyapeleka kwenye glasi ya kinywaji,akaona kama bia ilishaisha glasini,alikamata chupa ya bia na kumimina kiasi kwenye glasi ya bia.Hakuchelea aligugubia kama mikupuo miwili bila kuishusha mezani,alipomaliza akacheua kama mara tatu hivi,alihisi kilevi kikipanda vema ndani ya ubongo.Akajikuta akicheka mwenyewe

“Mimi ndiye.Mwingine hakuna”Alisema nakutizama simu yake.Aliiokota nakujaribu kupiga,simu aliyopiga iliita bila kupokelewa.

“Shiit.Kwanini hapokei?”alipayuka kwa ghadhabu.

Hakuchoka akapiga mara ya pli,iliita tena,akasikia ikipokelewa “Hallo Prety girl.Uko wapi mbona hupokei simu yangu?”

“Nakaribia jengo la Makutano hapa”

“Sawa. Nakusubiri kwa hamu wa moyo”Walikata simu.Mzee Jophu akawa habandui macho lango la kuingilia,alitaka kumwona Getruda akiingia kwa madaha.Ghafla aliona mlimbwende akiingia kwa mapana na kumfanya kila aliyeko mle ndani kumtupia jicho.Getruda hakuwa mzuri sana wa sura,lakini umbo lake na makalio ndio kichochezi kwa wanaume rijali.Kila alipovuta hatua ,makalio yake yalitikisika mithili ya mawimbi baharini.Nafiki jambo hilo ndilo lililomfanya Mzee Jophu ammezee mate mke wangu.Si kwamba na msifia kwa vile ni mke wangu,hapana.Njoo kwangu Arusha ushuhudie, ukweli wangu.Lakini kwa sasa ni mzee sana.

“Kaaaa, kakaka!”alionekana kijana mmja aliyeko nyuma ya mzee Jophu akihamaki,mfdomo ukiwa wazi kwa mshangao na mkono ukiwa umeshika mdomo wa chini,Jicho likiwa limemtoka kama ndulele iliyoiva.

“Mkindu wavona ilo ibora ledha aho”Kijana huyu alimwambia mwenzake kwa kilugha.

Akimaanisha “Mkindu umeona lisichana hilo linalo kuja hapo?”

“Nikirumo ilo!”Mkindu alijibu.

“Hilo ni balaa!” Wakacheka.

Mzee Jophu alimsindikiza Getruda kwa macho ya matamanio hadi alipomkaribia kabisa.

“Vipi.Mbona umechelewa ?”

“Mume bwege alikuwa akinichelewesha”Getruda aliongea akivuta kiti kilicho wazi.

“Achana nae.Ukisha mkabidhi fisi bucha unamatarajio gani?”

“Kuokota mifupa”Getruda alidakia.

“Hakuna kinachobaki.Fisi gani anakuachia mfupa!”Wakacheka na kupigana mabusu.Kisha akagonga meza.

“Muhudumuuu”aliita.

“Nakuja”sauti ilisikika kwa mbali kidogo.

“Kuja haraka.Watu wanapesa zao hazina pakwenda”Alisema akijiamini kabisa.Getruda alimtizama akagundua mzee Jophu alishaanza kulewa.

“Mpati wa moyo wangu kinywaji chochote anachotaka upesi”Muhudumu akaitikia sawa.

“Dada nikupatie kinywaji gani?”

“Henken ya kopo.Usisahau mrija tafadhali”

“Ya baridi au moto?”

“Aaaa! Vuguvugu.Nitapata?”

“Usihofu,utapata”Muhudumu aliondoka.

“Mpenzi nimekuita nina jambo muhimu la kukueleza,hivyo basi naomba uwemsikivu”Alitulia kidogo na kuokota glasi ya bia,hakuchelewa alimimina bia yote na kurudisha glasi tupu.Akacheua mara mbili nakuendelea “Kwanza kabla ya yote. Napenda unihakikishie kwamba unanipenda”

“Nakupenda sana mpenzi inamaana hujagundua bado?”

“Ninyi wanawake mnabadilika sana.Lazima kila tunapokutana tuulizane jambo hili”

“Si wote bwana.Unajua ninyi wanaume mkionyeshewa kama mnapendwa sana vichwa huvimba na kujiona mna matilaba ya kufanya lolote juu ya mwanamke”

“Ni baadhi ,si mimi Jophu”Akasema na kusogeza kiti jirani na Getruda.Kabla hajaendelea tayari vinywaji vililetwa,Henken ya Getruda na safari ya Mzee Jophu.

“Karibuni”Muhudumu alisema.

“Ahsante”Getruda akajibu.

“Wee binti mwite mchoma nyama tafadhali”Hakukawia kufika mchoma nyama. “Kata nyama ya kidari,ile laini…umeelewa?”

“Ndio,bosi”

“Haya futikaa”Alisema kiulevi ulevi.Akamgeukia Getruda, “Wife,sasa tuendelee na mazungumzo yetu”

“Kama umenidhihirishia unanipenda utakuwa upande wangu kwa lolote lile,si ndivyo”

“Ndivyo”

“Nikisema kitu kwa manufaa yetu lazima tusaidiane,sivyo?”

“Ndivyo”alijibu kiupole hakujua ni jambo gani anataka kuelezwa wakati huo.Kwa sasa Mzee Jophu akapunguza sauti akamweleza Getruda kwa sauti ya chini kabisa.Nafikiri alihofu watu kung’amua maneno yake.

“Getruda naomba iwe siri kubwa sana.Nataka tumuondoe Sweedy Duniani”Getruda alishituka sana kama aliyeamshwa usingizini. “Heee!”

“Usishituke laazizi wangu.Nimeamua hivyo kwa manufaa yetu pia.Kila siku kujiiba iiba ,tutajiiba mpaka lini?.Heri afe tupate uhuru….”

“Haiwezekani Jophu.Unajua dhambi ya kuua lakini?”Getruda aliuliza.

“Acha ujinga, nani kakuambia kuna dhambi.Nani aliyeenda akarudi akasema kuna adhabu kali?.Niambie”

“Kwenye maandiko takatifu,maneno hayo yapo.”Getruda alijibu akimtizama Jophu.

“Kumbe nimaandiko yaliyotungwa kama hadithi tu.Nitajie nani alikufa akafufuka na kutuonyeshea adhabu alizopata ahera?”

“Bwana acha mizengwe yako.Uhusiano wetu hauwezi kuzuilika kwa sababu ya Sweedy”

“Nitakupa chochote lakini tumuue Sweedy.Uko tayari?”Getruda alikaa kimya,safari hii alishindwa kijibu. “Nijibu basi?”Mzee Jophu alimhimiza.

“Nikujibu nini?”

“Kwani hujui.Sina jibu lolote.”Akamtizama Mzee Jophu ,na kuvutakumbukumbu ya siku ya kwanza tulipokuwa kanisani,alikumbuka maneno mengi ya mchungaji.Akanikumbuka nilipompiga busu la kwanza nikiwa namvisha pete ya ndoa.Pia akakumbuka maneno ya mama yake akimweleza juu ya unyumba wetu.Machozi yakamtiririka mashavuni bila kujijua.Akapandisha mkono wa kuume ulioshika leso na kujifuta. Mzee Jophu alinyoosha mkono na kumpatia funguo Getruda.

“Kuanzia dakika hii.Land cruiser iliyoko nje ni mali yako.”Getruda alishangaa hakuamini kile alichokuwa akikiona wakati huo.

“Mpenzi ni kweli ama ni mipombe inakusumbua akili?”

“Sijalewa wa moyo.Ninachohitaji sasa hivi, ni kutoa uhai wa huyu hanithi”Akatulia kama nukta tano hivi ,kisha akasema,“Sawa sawa?”

“Sawa”Getruda alijibu mapigo ya moyo yakimwenda mbio.Alifikiri na kuona kwanza alishachoka kukodi teksi kila siku.Naye alitaka kutembelea gari la kifahari.Alitamani akawatambishie mabinti wenziye aliosoma nao pale Mkuu Rombo.Watajuaje kwamba naye nitajiri pasipo kutembea na gari la kifahari?.Aliamini mtu akiwa na pesa huheshimika kuliko hata kitu chochote duniani.Akajikuta moyo ukipamba na furaha kali, “Acha afe bwana kwani nini bwana. Mtu kama furushi la nguo, heri afe , wangapi wameuawa na kuwaacha wake zao na mapesa kibao.Mungu nisamehe”aliwaza akilini.


Waliendelea kunywa na kula nyama choma pale.Getruda alimaliza bia yake na kuongezwa zingine mbili,tayari ubongo ukafa ganzi.Alianza kuongea sana,tena bila kujali kwamba alisikiwa na watu. “Mpenzi wangu nasema hivi…nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe.Haina haja ya kuishi wakati hana sifa ya kumfanya hai. Eti mume, mume gani bwege kilasiku hapandi kitandani mpaka nishikwe na usingizi ndio nae apande!!!!”

“Hatakama ingelikuwa mimi.Ningetumia akili hiyo hiyo.Unafikiri ni kazi ndogo hiyo…fedheha bwana!”

Mzee Jophu na Getruda alikunjwa na kuondoka zao.Walielekea nyumba moja ya wageni ambako waliingiza gari la Gertuda na kujipumzisha.


**************

Katika maisha yangu nina kijitabia fulani cha kutotoka siku za mwisho wa wiki,isipokuwa jioni tena nikiwa na mke wangu ,Getruda. Huwa natoka katika matembezi mafupi na kurudi nyumbani.Juma pili hii ilikuwa ngumu kwangu.Kwanza mke wangu hakuwepo,usishangae nikimuita mke wangu japo sikufanikiwa kufanya tendo la ndoa.Ni mke wangu kwa sababu nimefunga ndoa kanisani.

Mawazo bado yalinizonga sana akilini,niliwaza safari ya ghafla ya mke wangu.Nilitamani sana nijue maendeleo ya wazazi wake huko mkuu Rombo.Kingine ni tatizo linaloniletea utata ndani ya ndoa yangu.Nilizidi kuwaza ,kwanini ugonjwa huo uwe kwangu tu.Kwanini usiwe kwa fulani?.Nilitamani kunywa bia lakini lakini nikaona si kutatua tatizo zaidi ya kuliongeza.


Nikiwa kwenye dimbi la mawazo,nilisikia simu ikiita,nilishituka sana.Kwa haraka nikaiendea simu ambayo niliiacha Varandani juu ya meza.Nilifikiri mambo mengi ,nikahisi aliyepiga simu alikuwa mke wangu akinipa habari za mama yake,nilitegemea kupata habari mbaya kutokana na maneno aliyoniacha nayo Getruda jana alipokurupuka akionekana wazi kuchanganywa na hali ya mama yake.Nilipofika nikaiokota simu upesi na kuipokea , “Hallo mume wangu.Umzima ?”

“Ndio.Vipi kuhusu hali ya mama.Anaendeleaje?”Nilimwuliza.

“Kidogo amepata ahueni.Kuna uvimbe gotini unamsumbua”

“Utakuja lini?”

“Aaa kesho jioni.Namsaidia kumuuguza hospitalini”

“Sawa.Nimebaki mwenyewe kama mkiwa”

“Usijali mpenzi.Upo nyumbani, na hutoki leo?”

“Ndio,nipo sitoki bila wewe.Kwanza najisikia vibaya kabisa sijui ni kwanini mpenzi”

“Pole sana mume wangu,bye”

Getruda akakata simu.


*********************


Kulikuwa na kundi la patao watu watano,aliyekuwa msemaji mkuu akiwa mzee Jophu.Pembeni aliketi Getruda na kushoto kwake mwanaume mmoja mwanye umbo kubwa,unaweza ukamfananisha na mcheza mweleka.Mikono yake minene iliyojaa na kujengeka misuli.Kushoto kwa mwanaume yule alikuwepo kijana mwingine,mrefu mwembamba lakini anasura ya kukatili.Ukimuona lazima ungemtambua kama ni muuaji.Huyu aliweka bastola kibindoni,bastola aina ya Revolver.Aliyebaki alionekana mdogo sana,ukitadhimini umri wake ni miaka kumi na tano,alionekana alikulia mitaani.Huyu ni kibaka mzoefu ,achilia mbali bangi ,sigara na dawa za kulevya, kuvuta petroli na gundi ya viatu kwake si tatizo.Mtoto huyu walimtumia sana katika matukio ya ujambazi na upelelezi wa wapi kuna pesa ,wapi tukaibe leo.


Walicheka muda mfupi tu baada ya Getruda kukata simu, “Anasemaje huyo maiti”Mzee Jophu aliuliza akiwa anamtizama Getruda kwa udadisi.

“Anasema leo yupo nyumbani hatoki,ni jambo ambalo liko wazi bila mimi habandui mguu wake.Hivyo kazi yake imeisha”

“Patamu sana hapo.Naomba vijana wangu waingie kazini.Kama nilivyo waelekeza na mfanye kwa tahadhari sana msije kubainika kama ninyi ndio mlioua.Mmenisikia?”

“Mzee usitufundishe hii ndio kazi yetu kama kazi nyingine.Tumeua sana na tutaendelea kuua.Pesa ya kazi mbele”Alisema jambazi mmoja nene lenye kifua kama pipa,lilitambulika kwa jina moja tu ‘Man Kaugo’Man Kaugo ana kasumba moja hataki kufundisha kazi ya uuaji,nasema anaielewa vema na ujuzi huo kwake ume komaa.

“Naona mchukue lita arobaini za petroli.Mzungushie nyumba yake yote na muitie kiberiti”

“Eeee!kuna vitu vyangu vya muhimu.Kwanini msimuue bilakuchoma nyumba”

“Vitu vyako nitakulipa.Tatizo ni nini?”

“Nyumba yamgu.Nilitaka mumuue nibaki na nyumba”

“Nyumba nitakununulia njiro”

“Haya, usinidanganye mpenzi”

“Sikudanganyi.Mimi na wewe kwani wa tani?”

“Hapana”

“Sasa kumbe…” akatulia kidogo kisha akasema, “Nafikiri tumemaliza makomando wangu”

“Pesa zetu bado.”

“Kiasi gani ?”

“Milioni tatu kwa kichwa kimoja”

“Ok,subirini kidogo nakuja.”

Mzee jophu alitia gari moto na kuondoka zake.alielekea benki ambako alichukua milioni tano na kuzihifadhi.Hakuchelewa alirudi. “Kamata milioni tatu hizi.Naomba mharakishe tafadhali”

“Sawa mzee.Utasikia mwenyewe mambo yakijibu”Wale vijana waliondoka zao.

Nilisikia kama watu wakiongea nje ya jengo langu,kila nilipojaribu kutega sikio kwa makini,nilishindwa kun’gamua mazungumzo yao.Nilitunguza redio kabisa ,japo nilikuwa macho lakini nilihisi bado kiko usingizini,watu hao walinikaribia dirishani ,kwambali nikasikia mmoja wapo akisema “Hili ndilo dirisha lake”

Mwingine akasema “Basi hapa tumwage petroli nyingi iliafe haraka”kilikuwa kitendo cha haraka nilisikia petroli ikimwagwa dirishani,nilikurupuka na kushituka ,nilipofungua macho kumbe nilikuwa nikiota njozi mabaya kabisa.Kukurupuka kwangu hata mke wangu Suzan ambaye tulibahatika kupata mtoto wa kiume aitwaye Samji ,alinisikia nikipiga kelele, “Nakufaaaaa”

“Nini mume wangu?”Suzan, mke wangu aliniuliza akiwa na masalio ya usingizi.Nilihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio utadhani nilikimbia umbali mrefu bila kupumzika.

“Baba samji,ni nini mbona umepiga kelele kiasi hicho?”

“Ndoa yangu inanitesa”Niliropoka nikipikicha macho, sikuamini yale niliyoyaona nikiwa usingizini.

“Ndoa yako inakutesa kivipi?”

“Nafikiri nilikuwa nikiota ndoto ya mateso kabisa”

“Ndoto?.Nilikusikia hata wakati mwingine ukilia ukiwa usingizini.Nilikutingisha lakini huku shituika, ulikuwa ukisema Getruda Getruda .Getruda ninani?”Nilitulia kidogo nikajaribu kumkumbuka, “Getruda ni huyo mwanamke niliyemuoa, akawa ananitesa”

“Usinidanganye mume wangu.Madhambi unayofanya na mahawara wako ,ndio unayaota usiku?”

“Basi nisamehe mke wangu,ni ndoto tu.Sina mtu nimpendaye zaidi yako.Sijui njozi ya ajabu namna hii imetokea wapi.Yote niliyoota hakuna hata kimoja kilichowahi kunitokea”

Ilikuwa usiku ,majira ya saa kumi na moja.Suzan, mke wangu alinisamehe na tukaanza kusali.