Friday, July 20, 2018

Hataki nimpigie simu usiku Nifanyeje???


SWALI-Mimi ni msichana naishi Arusha, nilitokea kuwa na uhusiano wa kimapenzi na kaka mmoja ambaye baadaye nilizaa naye mtoto mmoja. Tangu nijifungue nina miaka minne, kipindi hiki chote hatukuwa na mawasilino na mzazi mwenzangu. Hivi karibuni alijitokeza na kutaka turudishe uhusiano wetu nikakubali. Lakini amekuwa hataki niwasiliane naye wakati wa usiku na kuna kipindi nikimpigia simu anakata. Nilipojaribu kumuuliza hakunijibu zaidi ya kuwa mkali, nimweleweje?

JIBU-Mdogo wangu mambo mengi yanayotokea duniani yana dalili zake, mvua ikitaka kunyesha kwa mfano dalili zake huwa ni mawingu, malaria nayo ina dalili zake. Hata tunapozungumzia usaliti wa kimapenzi kuna dalili zake ambazo ni pamoja na hizo za mtu kutotaka kuwasiliana naye. Lakini, wataalamu wanasema dalili huwa si tatizo bali hutumika kutambua tatizo. 

Kwa msingi huo, hatuwezi kumhukumu mpenzi wako kwa kutumia dalili za kutokuwa mwaminifu, nakushauri uwe makini naye na umchunguze kwa nini hataki kuwasiliana nawe. Ikiwezekana akupeleke nyumbani kwake na akupe uhuru wa kufika huko kama mzazi mwenzake wakati wowote. Lakini pia ni vema ukamuuliza kulikoni akuzuie jambo jema kama hilo la mawasiliano tena nyakati ambazo ni za kuliwazana? Maana mchana ndiyo watu huwa bize sasa usiku kulikoni? UKIMWI UNAUA!