Saturday, October 13, 2018

SIMULIZI - AHSANTE HAIKA

Hata kama waseme sana
Hata kama wanune sana
Hata kama wasuse sana

Alikuwa  ni haika , anateremka katika ndege ya shirika la ndege la Air Tanzania , uwanja wa ndege wa mwalimu JK Nyerere , uwanja ulikuwa umependeza sana kwa rangi zake muruwa , watu wamependeza kila mtu alionekana mwenye  sura ya amani na tabasamu , wengine walikuwa wanasafiri kwenda nchi mbali mbali , wengine walikuwa wanawanngojea ndugu zao na jamaa zao waliotoka safari za mbali .

Kulikuwa na kijana Juma , naye alikuwa sehemu ya wageni , yeye ni mgeni  uwanja wa ndege lakini ana mngoja mgeni mwingine anayeitwa haika , alikuwa anatokea huko mikoa ya  kanda ya ziwa shinyanga , Juma hakuwahi kukutana na haika hata siku moja kwahiyo kila mmoja alipenda kumwona mwenzake .

Wakwanza kumtambua mwenzake ni Haika , yeye ndio alienda kumshituwa Juma kwamba ameshafika na kuongea nao mambo machache , Juma alikuwa ameshachoka pale kwa sababu alikaa muda mrefu bila haika kufika akakata tama .

Ngozi yake ilivyokuwa nyeupe , mwili wake mkubwa kidogo ( chubby ) , tabasamu lake la bashasha , nywele zake ndefu mpaka mgongoni , mwendo wake wa twiga  , sauti yake tamu , na madaha yake ya mapozi yalitosha kumweka Juma katika kizaa zaa .

Basi Juma alivyonyanyuka kutaka kumpokea haika hakuna na uhakika afanye nini kwasbabu haika alikuwa amekamilika mwili wote kwa mambo ya urembo , anavyovutia na kuvutika , hata kama uko mbali kabisa , utajisikia uko majaribuni tu .

Mara alitaka amshika miguu yake kama alivyozoea , lakini akaona maziwa yake ni zaidi , alipoenda juu kutaka kushika maziwa , akaona kifua nacho kimejaa , mata hips , mara sura yake , sijui sauti yake mwishowe , sasa haika ndio alimshika Juma mikono , Juma alitetemeka kwa muda kabla hajatulia .

Kama mzaha vile , haika alikaa chini kasha akamvuta mkono Juma naye wote wakaketi chini katika viti vya wageni pale uwanja wa taifa , taratibu haika alishika shingo ya Juma akaivuta upande wake na akambusu .

Juma naye hakufanya mzaha alionekana ni mwenye aibu sana , naye akajisogeza zaidi , akamshika haika kiuno chake , akamsogelea zaidi naye akarudisha busu la madaha ndimi zao zikakutana .

Mpenzi naomba japo nafasi
Mpenzi naomba unipe japo nafasi , usiniweke roho yangu juu


Ulikuwa ni mchezo wa mabusu na ndimi kwa dakika 5 hivi , haika akaishiwa nguvu akalala kidogo katika miguu ya Juma kama vile ni mgonjwa au anahitaji huduma Fulani ambao kwa pale hakuna wa kumpa ni Juma pekee .

Kichwa cha haika kililala katika  mapaja ya Juma naye Juma akajilaza mgongoni mwa haika huku ameshika kiuno cha haika , walianza kuongea maneno machache , kisha wote walinyanyuka na safari ya kuondoka uwanja wa ndege ikatimia .

Walikuwa wameshikana mikono lakini wakait mwingine Juma alimshika haika kiuno chake , kama vile anambembeleza ilionyesha kwamba yeye Juma kitu anachopenda kwa msichana ni kushika kiuono au mauno ya mtu Fulani .

Wakatoka nje , haika akapanda katika gari ya Juma , safari ya kuelekea sinza ikafika , wote alikaa siti ya nyuma dereva alikuwa mbele ndio anaendesha gari kwahiyo mambo yalikuwa bam bam huku Juma na haika wake wanafanya mambo yao .

“ unafikiria nini kuhusu mimi Juma “

nafikiri wewe ni msichana bora duniani

“ ehh kweli Juma ? “ haika aliuliza kwa kutojiamini

ndio kweli wewe ni msichana wa pekee ndio maana tuko wote siku ya leo , kwani uliamini kama siku tutakutana ?

“ ohh ahsante sana , mambo mengine vipi ?”

salama tu nakusikiliza wewe , hapa mi ni mwenyeji kwahiyo sema ratiba yako tu

“ ahsante kwa mualiko wako “

wasalaam , karibu sana duniani , mmm h  mhh mpenzii

“ahaha , mpenzi tena ? “

ah usijali , niambie vp chuchu zako ?

Safari ya Juma na haika ilikolea , ilienda mpaka kimara , nyumbani kwa Juma , wote walienda  pale , haika akashusha mizigo yake , wakatulia kwa muda kisha wakaelekea chuo kiguu idara ya mahesabu na ukaguzi .

Haika aliona wengi sana , wakubwa kwa wadogo , vilema na vipofu , majaji na wahukumu lakini ameamua kutulia kwa Juma , moyo wake ulisumbuka sana kutokana na ule urembo wake , hakujua kwamba siku moja atakutana na kijana Juma atulie nae

Naye Juma alipata fahari sana awapo karibu na  mrembo haika walionekana kama vile wako katika ndoa tayari ila ndio hivyo siku za mwanzo mwanzo tu , na kwa hakika mtu angefanikiwa kufungua kifua cha Juma angeona kiwili wili cha haika mwilini mwake .

Wote haika na Juma hawakuwa na kipingamizi cha kuwazuia kuwa pamoja na kufaidi mapenzi yao jinsi wanavyotaka wao bila bugudha zozote kutoka watu  wengine kama wanavyofanyiana katika mahusiano yao .

Yupo kwa ajili yake
Hata kama haika akiwa mbali
Penzi lake hatolinadi
Hivyo ndivyo alivyo

Kwa dhati Juma alinena kutoka moyoni , na kumwambia mrembo haika , naye haika alikubali ukweli huo na kumuonya Juma kuhusu mambo kadha wa kadha kabla ya kuamua kuingia katika dunia yao wenyewe inaonyesha walikubaliana vizuri

Kwa muda ilimbidi Juma awe mvumilivu kidogo kwasababu haika alikuwa na mambo yake mengine ya kimasomo na kikazi kwahiyo aliachana na Juma walionana jioni tu , Juma naye alikuwa na mambo yake ya kazi pia .

Walikutana kwa muda mchache sana siku za kazi , wote walingoja siku ya weekend ndio wakae karibu tena zaidi na kuongea , kutembelea baadhi ya maeneo mazuri ya jiji la dare s salaam na bagamoyo .

Pia walitakiwa kwenda nyumbani kwa haika ili Juma apate kujuana na ndugu za haika angalau wachache kuweka uhusiano wao katika hali nzuri zaidi , na kuaminiana hiyo ndio ilikuwa mipango yao .

Haika hakuweza kuondoka bila Juma kwenda nyumbani kwao kujuwana na baadhi ya ndugu zake , naye haika alitakiwa kwenda kimara baruti kuonana na baadhi ya ndugu ya kijana Juma .

Hii ilikuwa na siku maalumu sana kwao na kwa hao ndugu zao , ilikuwa ni kuwekana wazi zaidi na kila mtu alikuwa na mambo mbali mbali ya kuongea katika mikotano hii miwili ambayo ni muhimu sana .

Jumamosi ikafika , Juma siku hiyo hakwenda kazini , naye haika hakwenda chuoni kwahiyo wote walikuwa wamejibanza kimara anapoishi Juma , muda wa saa 4 hivi walitoka kwenda chuo kikuu kwa ajili ya kuogelea na kufanya mazoezi .

Mrembo haika alikuwa muoga sana wa maji , sio kwamba hajui kuogelea au hajawahi kuoelea bali hajaingia katika bwawa la kuogelea kwa muda mrefu , na hii ilimtisha sana , alihisi anaweza kuzama au labna anaweza kusahau kuogelea .

Yeye Juma hakuwa na wasi wasi wowote kwasababu ndio mazoea yake kwenda kuogelea pale kwa masaa 6 kila jumamosi na jumapili , ukijumlisha unapata masaa 12 ya kuogelea kwa wiki moja .

Ilibidi waanza kufundishana na kukumbushana baadhi ya vitu katika bwawa hilo , macho yote yalikuwa upande wao , tatizo lilikuwa kwa haika ambaye ndio alikuwa kinara wa urembo pale .

Kila anayeogelea wale wanaume walipenda nao waende kumfundisha kuogelea na kumkumbusha baadhi ya mambo , waliokaa njee walimshangaa na kumtamani mwili wake , wengine walikuja kabisa pale kusema kwamba amewavutia .

Wengine waliomba kupiga naye picha wakati anatoka zake kuogelea , wengine waliomba mawasiliano naye kama simu , email na vitu kama hivyo , lakini bahati mbaya maombi ya simu na email yalikataliwa walipiga naye picha tu .

Muda wa kuogelea ukaisha , Juma alienda chumba cha kubadilisha nguo cha wanaume naye haika alienda kwa wanawake , kisha wote wakatoka nje , kupakia usafiri mpaka nyumbani kwa wakina Juma .

Nyumbani kwa wakina Juma walimwandalia haika mambo mazuri na matamu , haika alishtuka tu hakujua nini kinaendelea kwanini watu wanampigia vigelegile , Juma alikuwa anatabasamu wakati wote , alimshika kiuono haika wakawa wanatembea .

Kabla ya kufika katika gorofa ya nyumba kubwa , Juma alimnyanyua haika na kumbeba na mikono yake , akampitisha mlangoni mpaka sebuleni akamweka katika kiti , pale alianza kuwatambulisha baadhi ya watu waliokuwepo .

Ndugu , jamaa , marafiki na majirani walifurahi sana , walionyesha furaha ya wazi kwa wapenzi hawa wapya , walipewa mkono wa pongezi , baba  yake Juma alimshukuru mungu kwa kuleta msichana bomba , mrembo na anayevutia katika familia yao .

Haika kama anayoeleweka sio mtumiaji wa vilevi , hivyo hivyo kama mwenzake Juma , wote walitumia vinjwaji laini , lakini watu wengi walitumia pombe na mambo mengine mazuri kwa maisha yao ya kila siku waliyozoea .

Baada ya kujuana na wazazi wa Juma nakukaaa pale kuongea sana , vijana Juma na haika walifungua dansi la kuondokea , kidogo kuburudisha jamii iliyowazunguka na kuweka historia kidogo ya mambo yao mazuri na matamu .

Nyimbo hiyo ilikuwa inaitwa “ YOLELE “ imeimbwa na Papa Wemba , nyimbo ya mahadhi ya  afrika ya kati na karebean , kwahiyo walicheza na kuserebuka mwishoni wakamalizia na nyimbo inayoitwa “ HAVE I TOLD U LATELY “iliyoimbwa na rod sterwat .

Kama mzaha Juma alimbeba tena haika , na kumkimbiza katika gari , kisha akaja kuwaambia wageni waalikwa na watu wengine pale ameondoka naye wasije kumpenda zaidi wamnganganie kubaki pale .

Ilikuwa ni kicheko kidogo kwa watu wengine , ila kila mmoja ana mawazo yake kwahiyo mambo ndio yalienda hivyo , saa 12 alikuwa wameshatoka pale kwa wakina Juma .


Wakawa wanaelekea kati kati ya jiji , katika hoteli seacliff , kwasababu Juma ni mpenzi wa michezo ya karata na kamari katika hiyo casino ya seaclif hotel , hapo hotelini Juma alikutana na rafiki yake wa shule anayeitwa Farid na watu wengine wengi tu .

Haika hakujua nini kinaendelea yeye aliwekwa chumba maalumu aliambiwa kwamba Juma ameenda katika mkutano kidogo , ila haika hakuhoji ameenda katika mkutano usiku ? tena bila taarifa maalumu ?

Ukweli ni kwamba Juma alikuwa chumba cha pili tu toka pale haika alipo na kwanza alikuwa anamuona haika katika kioo akiwa kile chumba cha pili lakini haika hawezi kuona kwasabab ya vile vioo maalumu vilivyowekwa pale .

Mara nyingi watu wanaocheza kamari au watu wanaojihusisha na michezo ya kamari ni wapole sana , wacheshi sana halafu ni watu wanaokosa raha muda mrefu kwa sababu muda mwingine wanafikiria kuhusu michezo ya kamari kushinda tu .

Wengi huwa wanajua kidogo kama sio sana michezo ya mapambano kama karate na kung fu kwasababu katika kamara kasheshe zaweza kutokea na watu wengine huwa na walinzi wao wa kuwatetea

Huwa wanatamani kusiwe na mchana , yaani siku zote wawe wanacheza kamara wanavyotaka hata kama wakiwa masikini wakutupwa ila wapate nafasi ya kucheza kamari kidogo wanavyotaka na ndio kijana Juma alivyo .

Mcheza kamari Juma ni kijana mcheshi sana akiwa na watu anaojuwana nao , mpole sana akiwa mwenyewe au sehemu yenye watu wengi na ni mchezaji mzuri wa mchezo wa kung fu , pia hana raha wakati wote kwa sababu anahisi kama Fulani amemshinda katika mchezo wa kamari .

Mkupuo wa kwanza katika kamari ulipita na Juma alishinda , akatoka zake pale ukumbi wa kamari na kwenda kumwangalia malkia wake aliyekuwa mpweke amekaa mwenyewe pale , alipofika pale aliinama kidogo akampiga busu kisha naye akakaa chini .

“ eh sema , huo mkutano unafanyika usiku kwanini ? umeshamaliza ?”

ahaa usijali hapana haujaisha nimetoka mapumziko kidogo sikia chukuwa hizi hela ukitaka chochote ununue sawa ?” Juma alimwambia haika

“Kama sitaki kitu je ? “

ohh sasa kama hutaki kitu ni balaa naweza kuchelewa kutoka raundi ya pili mpenzi

“ basi nipe nafasi niende zangu kama ndio hivyo “

la hapana huwezi toka mwenyewe manake hapa ni balaa wife .

“ balaa gani  ? “

sikiliza nkwambie , ukweli , kule ndani nacheza kamali kidogo !!!

“ yesuu wangu “

sasa yesu wa nini hapa ? kwan tuko kanichani ?

Alipomalizia kusema hivyo tu , ghafla vijana 4 wakaingia pale katika chumba ambacho Juma na haika walipokaa , wote walivaa suti nyeusi na miwani myeusi , hawakusema wanataka nini pale alizunguka tu meza .

Ndio mzee mmoja akaingia ndani naye , huyo mzee akamwambia Juma alete zile hela alizoshinda katika mchezo wa kamali kule ndani kama anataka kuondoka au arudi kuendelea kucheza mpaka round ziishe .

Ombi hilo lilikataliwa na kijana Juma , kwahiyo yule mzee alinkunja shati na kumnyanyua juu kumsimamisha , haika alianza kulia hapo hapo huku ameegemea chini ya ile meza hakujua afanye nini .

Ushupavu wa Juma ulianza kuonekana pale alipoushika mkono wa yule mzee na kuugeuza , kisha akamshika kichwa chake akakipigisha juu ya peza ile ya vioo , ikaliaa poooo, kioo kikavunjika vipande vipande , kisha akamkaba koo kumshikilia kama mateka .

Hapo wale vijana wakashindwa wafanye nini kwasababu bosi wao alikuwa ameshatekwa , Juma na haika walitoka ndani taratibu huku wamemshikilia yule mzee , wakaingia katika gari yao , wakawasha gari kisha wakamwachia yule mzee .

Kizee kikawa kinakimbilia tena kule hotelini , Juma bila huruma alinyanyua pistol yake toka katika kiti cha gari na kumpiga yule mzee risasi  2 moja ya kisogo na ingine ya mguu , maisha ya yule mzee yalimalizwa hapo hapo .

Its me against the world
Its me against the world baby
I got nothing to loose

Huku nyuma yake , dereva aliondoa ile gari kwa spidi kubwa sana , haika alikuwa bado analia kwa uchungu na uoga ulijijengea kwake , safari iliendelea kama kawaida lakini kwa spidi ya juu sana .

Mpaka kimara wakafika , wakaingia ndani kujifungia na kuanza kuuchapa usingizi , mrembo haika bado hakuamini kilichokuwa kinaendelea , kwanza hakuamini kama ametoka salama mikononi mwa wale jamaa waliozunguka meza yao .

Paaaa  “ sa ndio imenifanyia nini vile ?” haika alimpiga kofi Juma kwa hasira
thiijui kwatha pumthika kwa amani thitaki matatitho thaa hithi .

“ nipumzike ? mimi nipumzike ? “

Ndio veve , au ntoke nkuache hapa meyeve ?

“ haya toka kama unaweza “

Huyoo Juma kwa huzuni aliinamisha kichwa chake chini akatoka zake nje , akamwacha haika chumbani pale , Juma akakaa zake sebuleni usingizi ukamshika na akalala pale pale sebuleni .

Katika saa 9 hivi za usiku haika akaamka kwenda kumwangalia Juma alipo akamkuta amelala chini sakafuni , ikambidi aende kuchukuwa maji ya baridi bafuni , kisha akaja zake pale akamwagia ili aaamke .

“ sasa ndio mambo gani unafanya dear ?”

si nimekuamsha ? twende kitandani bwana usijali

“ kwani umeshindwa kuji kunishika tu niamke ?”

nakupenda sana nimeona nikushangaze kidogo amka bwana twende .

Kwisha kazi ilionekana hasira za haika zimeshakwisha na ule mshituko alioupata , wakati anakuja kumwamsha Juma kwa njia ile haika alikuwa mtupu nguo zake zote aliacha zake kule chumbani .

Taratibu haika alimshika mkono Juma , wote wakaenda bafuni , kule bafuni Juma alienda kuogeshwa na haika mpenzi wake , baada ya kuoga wote wakaingia chumbani mwao kujiandaa na masaa yaliyobakia usiku huo .


Taa ilienda kuzimwa na haika , naye Juma alinyatia , wakati anataka kuzima ile taa , alishangaa mkono wake umezuiwa na Juma aliyekuwa nyuma yake , aliuvuta ule mkono na kuuweka mabegani mwake kisha akambusu .

Mikono ya  Juma ikashika kiuno cha haika , haika alikuwa anafanya kama vile kutingisha mauno yake kukatika , kisha wote wakapeleka mikono yao katika switch ya ukutani na kuzima ile taa .

Mikono hiyo hiyo ya Juma ilimbeba tena haika kwenda naye kitandani , akamlaza kitandani , Juma alitoka tena kitandani pale akawasha muziki , nyimbo iliyoanza inaitwa “ LOVE SCENE “ imeimbwa na Joe Thomas .

Lets make a love  scene
Lets make a love scene koz the night is so true
Coz I got what u want
You got what I need

Hakuna kitu kizuri kama umetoka katika matatizo halafu mpenzi wako anakusamehe , kisha akufungulie roho yake , mwili wake na maisha yake , utapata faraja sana utajisikia kama wewe ndio pekee hapa duniani .

Moyo wako unatakiwa ujue kwamba kuna mtu anakupenda zaidi , moyo wako unatakiwa ujue kwamba kuna moyo mwingine ambao unahitaji ushirikiano na ukaribu zaidi wa kimapenzi kimahaba na kila kitu kuzuri .

U will see I can give u , everything u need
Let me be the one to love u moreee

Kwa hawa wawili moyo wa Juma ulishajua dhahiri kwa kuna mwingine ambaye ndio huyo haika na haika kwake ilikuwa ni hivyo hivyo , maisha yalienda vizuri na salama kabisa .Bubu taka sema .

Usiku wao ulinoga sana kila mmoja alimwonyesha mwenzake anachojua ,kila mmoja alijitahidi kumridhisha mwenzake katika mambo matamu ya mapenzi na mahaba vijacho viliwatoka na kutiririka ingawa usiku huo ulikuwa wa baridi huu .

Kijana Juma alimlamba  mrembo wake kama pipi inavyolambwa au chatu anavyolamba lamba , ile miziki iliyokuwa inadondoka toka katika redio ndio iliongeza utamu wa penzi lao usiku huo liwe tamu zaidi na kuongezeka chachu .

Walinyonyana kama mtoto mchanga anavyonyonya dole gumba , yote hiyo ni ishara ya mapenzi na upendo uliojaa ndani ya vijana hawa wawili machachari Juma na mpenzi wake wa kichaga haika .

Asubuhi ikatimia haika akajiandaa kurudi zake kwao  alipotoka hapo mwanzo naye Juma kama kawaida yake alimpeleka katika uwanja wa kimataifa wa mwalimu nyerere kwa ajili ya safari yake .

Kwa hakika penzi huwa zuri na lenye neema tele haswa ukimpata mtu mliyeshibana naye mtu asiyedanganya kitu katika uhusiano wenu , mtu huyu sio mchoyo katika mapenzi kukuonyesha mambo mapya na mazuri siku zote unapokutana naye .

Nahisi siku ingine haika na Juma wakikutana basi mapenzi yao yataiva zaidi na kukuwa zaidi , siku hiyo haika atakuja tena dare s salaam wakati wa likizo yake ya kazi naye Juma atakuwa na off fupi ya wiki moja hivi .

LEO NI HARUSI YA HAIKA – NAMTAKIA HARUSI NJEMA NA MAISHA MEMA YA NDOA