Wednesday, October 3, 2018

Matumizi ya asali na ukwaju katika kuondoa chunusi

Matumizi ya asali na ukwaju katika kuondoa chunusi

Ukitaka kuondoa chunusi usoni na kusafisha uso usiwe na madoa ni vyema ukatumia njia asili kufanya hivyo tumia asali na ukwaju kupata matokeo mazuri bila madhara

Ukwaju na asali hupatikana kwa urahisi sokoni

Ipende ngozi yako wakati wote kama utaona inakuchukua muda mrefu kutengeneza mchanganyiko wa asali na ukwaju basi ni vyema vipodozi unavyonunua kama sabuni ama losheni hakikisha vimetengenezwa kwa mchanganyiko wa asali na ukwaju

Tafuta ukwaju loweka katika maji ukishalainika changanya na asali, paka usoni. muda mzuri wa kufanya hivi ni usiku  ambapo unapaka na kukaa takribani kama nusu saa kisha safisha uso wako vizuri fanya hivyo mara kwa mara kwani ni dawa nzuri sana na utaona ngozi yako inabadilika kwa kipindi kifupi.