Wednesday, January 10, 2018

Wewe ni mwanamke wa aina gani kitandani? kama unataka kuwa fundi kitandani hii isikupite




Mimi siyo muangaliaji wa mikanda ya kikubwa kivile, lakini nakumbuka wakati nikiwa shule ya sekondari wakati huo nikiwa bado sijaguswa niliwahi kuangalia mkanda wa kikubwa nyumbani kwa rafiki yangu wakati huo wazazi wake walikuwa hawapo. Kitendo cha kungalia ule mkanda kiliamsha msisimko wa ajabu kiasi cha kutamani nijaribu siku moja, lakini hata hivyo nilijawa na hofu. Je nikipata mimba nitamwambiaje yule Mzee Batash baba yangu mzazi, je nikipata ukimwi au maradhi ya zinaa, je maisha yangu ya baadaye yatakuwaje nikishindwa kuendela na masomo baada ya kupata mimba, ilimradi hofu hofu hofu.

Wakati huo nakumbuka kulikuwa na kijana mmoja tulikuwa tunasoma naye alikuwa akinifuatilia sana. Alikuwa ni kijana mzuri kwa sura, mtanashati na mtaratibu,lakini nilimwambia asubiri tumalize masomo yeye akiwa amenitangulia mwaka mmoja mbele, wakati huo nilikuwa kidato cha pili na yeye cha tatu.Nilipofika kidato cha nne, ndipo nilipopoteza bikra yangu baada ya kufanya tendo na yule kijana baada ya kujifanya mgonjwa simba.

Ilikuwa hivi.

Siku moja yule kijana alimtuma mdogo wake wa kike kuja kunijulisha kwamba anaumwa, nilipatwa na wasiwasi kuhusu hali yake nikakata shauri nikamuone kwani kwao hapakuwa mbali sana na kwetu, kumbe siku hiyo wazazi wake walikwenda shamba kijiji cha jirani, kitendo cha kufika nyumbani kwao na kuingia chumbani kwake hakikuniacha salama, alinishawishi kwa namna ya ajabu tukajikuta tumefanya.

Siku hiyo tendo halikuwa la burdani kwa sababu alikuwa na mihemko na miye nilikuwa na hofu, lakini baada ya kufanya mara mbili mara tatu, sikuona ule utundu na ufundi wa kwenye mikanda ya kikubwa, nilikuwa na matarajio makubwa ya kupata msisimko na raha niliyokuwa nikiona kwa washiriki wa kwenye ule mkanda wa kikubwa waliyokuwa wakiipata.

Nilifanya udadisi kwa wasichana wenzangu kuhusu jambo lile, wakaniambia kwamba wale wanaoshiriki kwenye zile filamu za kikubwa wanakuwa wana andaliwa na ile mikanda inarekodiwa kwa ufundi na kisha kuhaririwa, kwa hiyo kunakuwa nusu uongo na nusu ukweli.

Nilipomaliza kidato cha sita na kujiunga na chuo, pale chuoni kulikuwa na darasa la mazoezi ya viungo na ya kuchangamsha mwili wenyewe wanaita aerobics. Kushiriki kwangu katika yale mazoezi kuliufanya mwili wangu kuwa mwepesi na mtepetepevu yaani flexible.

Hapo chuoni nilikutana na kijana mwingine tukawa na mahusiano, kwa mara ya kwanza niliposhiriki tendo niliona tofauti kubwa. Kwani ushirikiano ulikuwa ni wakiwango cha juu na nilihisi kupata ile raha isiyo ya kawaida na ambayo sikuwahi kuihisi hapo kabla. Nilikuwa najiwa na matukio ya ule mkanda wa kikubwa niliouona kwa shogangu wakati ule na kila nilichojaribu kufanya katika kuiga walivyokuwa wakifanya kwenye ule mkanda nilijikuta nikimudu kwa ustadi wa hali ya juu huku nikipata ushirikiano mahiri kwa mwenzangu. Kusema ukweli nam-miss sana yule mpenzi wangu ambaye kwa sasa yuko ughaibuni kutafuta maisha.

Kuanzia hapo nikajua kwamba kufanya tendo ni Sanaa na linahitaji ushirikiano kati ya wawili, lakini pia ni vyema kufanya mazoezi ya viungo ili kuondoa ugoigoi kitandani, la sivyo utaishia kuona kwenye mikanda ya kikubwa au kusimuliwa na wala hutoweza kufikia kiwango cha raha inayopatikana katika tendo.

Kwahiyo tendo siyo la mtu mmoja bali linahitaji team work.