Wednesday, November 15, 2017

Kabla Ya Kuamua Kumchunguza Mwenza Wako Hakikisha Una Ubavu Wa Kumuacha



Kuna watu utakuta mume au mke akiweka simu tu chini wanaanza kuchunguza, kuangalia sms, wakikosa waaangalia simu zilizopigwa na wakiokosa huanza kuchambua majina ya jinsia tofauti yaliyopo katika simu za wapenzi wao.

Lakini hawaishii hapo, wakimuona tu mwenza na mtu wa jinsia tofauti hunza kupaniki na kutafuta namna ya kumfumania. Wewe endelea tu kutafuta na kumfuatilia, utapata unachokitaka, lakini swali linakuja ukishapata?
Unapomfumania mwenza wako unakuwa umejithibitishia kua hauko peke yako, utataka kuombwa msamaha na kutaka mwenza wako abadilike? Lakini hembu kabla hujaanza kumchunguza jiulize, hivi ukamfumania, akakataa kuomba msamaha au akaomba lakini akagoma kumuacha huyo anayechepuka naye utafanyaje?
Je upo tayari kuondoka na kumuacha? Kama jibu ni ndiyo endelea kumfuatilia lakini kama jibu ni hapana basi acha kabisa. Utajiumiza bure na kwakuwa utakuwa ushamfumania na kumsamehe bila hata kuombwa msamaha basi utakuwa umempa tiketi ya kuendelea naye.
Iko hivi mwanzoni alikuwa akichepuka kistaarabu, akijificha kwakuwa hujui. Lakini ukishamfumania akakuambia hayuko tayari kumuacha na wewe ukakomaa naye basi nisawa na umemruhusu, kwani hataogopa tena kufumaniwa mara ya pili.
Kwa maana hiyo wewe utaendelea kuumia na kila mara akitoka utajua yuko kwa fulani. Kama huna ubavu wa kumuacha hembu acha kumfuatilia maana utajiumiza bure, mfuatilie mtu kama unataka kumuacha zaidi utakuwa unahalalisha mke au mume mwenza tu.