Saturday, October 28, 2017

ZIFAHAMU FAIDA 10 ZA POMBE KWENYE MWILI WA BINADAMU....

pombe ni nini?
pombe ni neno ambalo linajumuisha aina zote za vilevi unazozifahamu, pombe za aina mbalimbali zinatengenezwa na kutumika na jamii zote duniani japokua kuna baadhi ya dini haziruhusu pombe. historia ya pombe inaonekana kwanzia zamani sana, kibiblia hata kabla ya kuzaliwa kwa yesu. sasa pombe ina hasara nyingi ambazo kila mtu anazifahamu ikinywea kwa kiasi kikubwa lakini kuna faida zake muhimu iwapo zikinywewa kwa kiasi kinachotakiwa.
kiwango sahihi cha pombe ni kipi kiafya? 
kitaalamu mwanaume mmoja anatakiwa anywe vinywaji viwili vya pombe wakati mwanamke anatakiwa anywe kinywaji kimoja cha pombe. sasa tunaposema kinywaji hatumaanishi chupa pombe ila tunamaanisha kiasi cha pombe na asilimia zake ndani.
kinywaji kimoja ni tunachozungumzia ni kama ifuatavyo...

  • milimita 354 za bia ya kawaida yenye 5% ndio kinywaji kimoja.
  • milimita 147 za wine au mvinyo yenye 12% ndio kinywaji kimoja.
  • milimita 44 za pombe kali kama viroba zenye 40% ndio kinywaji kimoja.
mfano hai tunaweza tukasema mwanaume anatakiwa anywe bia mbili tu kwa siku huku mwanamke anatakiwa anywe moja kama hizo kwa siku..
  • mwanaume anatakiwa kunywa nusu glass ya wine wakati mwanamke anatakiwa anywe robo glass ya  wine kwa siku.
  • mwanaume anatakiwa anywe robo glass ya pombe kali wakati mwanamke anatakiwa anywe theluthi ya pombe kali kwa siku.
  • sasa baada ya kuona kiwango maalumu cha kiafya ambacho mtu anatakiwa kunywa basi hebu tuone faida za kunywa kiasi hicho...
pombe hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo; utafiti ulofanywa na chuo kikuu cha marekani kwa jina la havard umebaini kwamba unywaji wa pombe kwa kiasi huongeza aina fulani ya lehemu nzuri inayoitwa high density lipopoprotein, lehemu hii hulinda moyo lakini pia pombe hulainisha damu na kuifanya iwe nyepesi hivyo kupita kirahisi kwenye mishipa ya damu na kuzuia presha na kiharusi. lakini pia katika hatua fulani ya ugonjwa wa moyo, mgonjwa huandikiwa kutumia pombe aina ya red wine angalau robo au nusu glass kwa siku.
huongeza urefu wa maisha; chuo kikuu cha catholic nchini marekani katika moja ya tafiti zake kiligundua kunywa pombe kiasi huongeza urefu wa maisha kwa asilimia 18 kuliko wale wasiokunywa, pia wakaongeza kwamba kunywa pombe na chakula ni moja ya njia nzuri sana ya kupata faida hii muhimu.
husaidia nguvu za kiume; jarida la jounal of sexual medicine liliandika kwamba wanaume wanaotumia pombe walipungukiwa na tatizo la nguvu za kiume kwa 25% kuliko wasiokunywa...lakini pia watu wanaokunywa pombe ni mashaihidi wa hili kwamba hata muda ule ukiwa umekunywa pombe, hamu inakua juu sana na ukipata mwanamke unafanya vizuri zaidi kuliko ukiwa hujanywa hii ikiwemo pamoja na kuchelewa sana kufika kileleni na kua na uume wenye nguvu sana kuliko kawaida..
hupunguza hatari ya kupata kisukari; unywaji wa pombe kwa kiasi huongeza uwezo wa homoni ya insulini kufanya kazi na hii hupunguza hatari ya kupata ugonjwa hatari wa kisukari, habari hii ilitolewa na kituo cha utafiti huko uholanzi..
hupunguza uwezekano wa kupata ugonjwa wa akili; utafiti uliofanyika kwa watu 365000 tangu mwaka 1977 na shirika la kimarekani, lligundua kwamba wanywaji wa pombe kwa kiasi kidogo kwa siku hawakuugua magonjwa ya akili uzeeni kwa asilimia 23 ukilinganisha na wale wasiokunywa kabisa.
huzuia hatari ya kupata mawe ya nyongo; ugonjwa huu unaitwa kitaalamu kama gallstones, watafiti katika chuo kikuu cha east ganglia walionyesha kwamba wanywaji wa pombe kidogo hawasumbuliwi na sana na ugonjwa huu kama wasiokunywa kabisa.
pombe ina madini muhimu ya mwili; bia nyingi zina vitamin b nyingi yaani thiamine na riboflavin, lakini pia zina calcium na magnesium nyingi ambayo ni muhimu sana kwa jili ya kazi mbalimbali za mfumo wa mwili wa binadamu.
pombe ni nzuri kwa wanawake zaidi ya miaka 50; baada ya umri wa miaka 50 mwanamke huanza kupata dalili za kupungua kiasi cha homone mwilini kitaalamu kama monopause, utafiti unaonyesha kwamba kemikali ndani ya bia zinaweza fanya kazi ya kuondoa dalili za homoni kidogo mwilini kama joto, mgandamizo wa mawazo na kadhalika.
huongeza kumbukumbu; kama wewe ni mnywaji, mara nyingi ukinywa unaanza kukumbuka mambo ya zamani sana na wakati mwingine kufadhaishwa au kufurahishwa na habari hizo. vivo hivyo ndio uwezo wa kumbukumbu zingine muhimu za kazi na kusoma zinavyoongezeka..
husaidia figo; jarida moja la kimarekani kwa jina la clinical journal of american society liliandika kwamba wanywaji wa pombe kiasi wanapungukiwa hatari ya kupata mawe ya figo kwa asilimia 30 kuliko wale ambao hawanywi, hii ni sababu ya kukojoa sana na kusafisha mafigo..