Friday, October 27, 2017

HAYA NDIO MAMBO 10 YA KUZINGATIA KWENYE MATUNZO WA UUME.....

kuhifadhi uume wako kwa usafi, mvuto na afya ni swala la kipaumbele kwa wanaume, kiungo hichi cha uzazi ni muhimu sana kwani ndio tofauti kubwa kati ya mwanaume na mwanamke, hata ukiwa baunsa na nguvu sana kama uume wako hauutunzi vizuri wewe ni bure tu. mambo yafuatayo ni muhimu kwenye kutunza uume wako.

  1. safisha uume wako na maji ya uvuguvugu angalau mara mbili kwa wiki, safisha korodani, safisha shingo la uume, kichwa cha uume na shingo lake kisha sugua taratibu korodani zako bila kutumia nguvu.
  2. kuacha nywele nyingi sio vizuri, zinaweza kukata ngozi ya uume au uke wakati wa tendo la ndoa, huweza kukata na kupasua kondomu, huleta harufu mbaya na hua chanzo kikuu cha majipu ya sehemu za siri.
  3. usiapuuzie ugonjwa wa uume wako, ukiona upele, jipu, mabadiliko ya rangi au hali  yeyote ambayo sio ya kawaida nenda ukaonane na daktari haraka sana ili upate suluhisho la tatizo linalokusumbua.
  4. wanaume wengi wana tabia ya kuvaa boksa moja wiki nzima au hata mwezi mmoja kabisa, hii inasababisha harufu kali sehemu za siri ambayo haitoki kirahisi. hebu nunua boksa mpya za jumla sokoni uwe nazo hata kumi ila kila siku unavaa boxer safi.[epuka boksa za mtumba ni hatari sana]
  5. chakula unachokula kina madhara kwenye ubora wa mbegu zako, epuka matumizi makubwa ya vitunguu swaumu, pombe, kahawa, vitunguu na viungo vya chakula. kula matunda yenye sukari ya asili kama maembe, maepo,machungwa na kula asali pia.zinafanya mbegu zako ziwe vizuri na kutoa mtoto mwenye afya.
  6. usitumie urembo wowote kwenye uume kama pafyumu, poda au manukato yeyote ya kufanya panukie. uume hautakiwi unukie, hiyo ni sehemu ya kazi tu. unaweza kusababisha michubuko na magonjwa ya ajabu.
  7. epuka kutumia dawa za kunyoa nywele kwenye sehemu zako za siri, zile dawa zina kemikali nyingi ambazo zinaweza kuharibu utengenezaji wa mbegu zako na kukuletea kansa na magonjwa mengine ya ajabu.tumia mkasi au mashine kunyoa.
  8. kama mwanaume vaa boksa ambazo zinakuachia hewa na ubaridi wa kutosha sehemu za siri, boksa zinazobana sana au uvaaji wa nguo nyingi huleta joto sana kwenye korodani na kuzuia utengenezaji wa mbegu za kiume.
  9. chagua kuvaa boksa zaidi kuliko chupi kwani boksa huacha uume wako ukiwa huru na hata ukuaji wa uume wako unakua mwepesi. watu wengi wanaovaa chupi wana uume uliopinda sababu ya kuulazimisha kulala upande fulani kila siku na hata ukuaji wa uume unazuiliwa.
  10. hakikisha umetailiwa ili uweze kujikinga na magonjwa mbalimbali ikiwemo ukimwi, kama hujatailiwa basi vuta ngozi kwa nyuma na uoshe uchafu wa ndani ya uume kila siku.
     kumbuka; uume ni mtukufu kuliko hata upanga wa goliati yule aliyepambana na daudi, lakini mwisho kabisa hakikisha unajifunza kugundua mabadiliko yeyote ya uume wako...inaweza kua ni kansa ya tezi dume ambayo inashika wanaume wengi zaidi ya miaka 50. kansa ya tezi dume ni halisi na inaua watu wengi sana duniani.
kumbuka hii makala sio matusi ila ni elimu, shea kwa rafiki zako wa kike na wa kiume waweze kusoma makala hii na kujifunza.