Monday, July 23, 2018

KUOLEWA NI NDOTO KUU YA KILA MWANAMKE ALIYEKAMILIKA ILA KAMA UNA TABIA HIZI UTAZEEKEA NYUMBANI


1. Tamaa ya utajiri, fedha na mali nyingi pasipo kutambua kuwa vitu hutafutwa.
Hapa wengi hupoteza nyota zao kwa kuwakataa wanaume wenye kipato cha kawaida na kujirahisisha kwa wenye nazo ambao kwa bahati mbaya wengi wao sio waoaji bali ni wahuni tu na watu wa anasa na kula bata mjini.

2. Dharau, maringo, kiburi na mashauzi classic.
Yaani we kila mtu akikusogelea na kujaribu kuzungumza na wewe unaanza kumpandisha na kumshusha kisha unamsonya. Wengi huishia kukupotezea wakijua labda umewadharau au tayari una mtu wako ndio maana una nyodo nyingi.

3. Huna Jumapili wala Ijumaa, yaani huendi kanisani wala msikitini, husali wala humuombi Mungu hakika lazima wahuni watapata nafasi kwako na kukuchezea mpaka uchakae kama mitumba wa ya mnadani.
MUNGU NI NGUZO KUU YA BARAKA ZAKO ukimuomba hakika atakuepushia kuingia midomoni mwa dubu na fisi wanaokuvizia na kuja kama malaika. Atakupa ufahamu wa kuwatambua na kuwashtukia mapema.

4. Kuvaa nguo za ajabuajabu kama changudoa.
Sijui ni nani aliyewaambia kuwa mkivaa hivyo mnapendeza! Unakuta binti kavaa kama mcheza show za night club, yaani akipita nguo inaonesha kila kitu na akiinama ndio balaa kabisa yaani kimini kinafunua kila kitu nje nje. Kwa staili hiyo nani atakupeleka kwao?

5. Kujipaka mirangi ya ajabuajabu usoni kama mwali wa kimakonde au kizaramo eti wenyewe mnaziita make-ups. Kwanza mnatutisha tu.
6. Kupenda kujirahisisha au kujipendekezapendekeza kwa wanaume, yani ukiguswa kidogo tu twende.
7. Kuwa na picha karibia 500 Facebook, Twitter, Whatsapp n.k halafu picha zenyewe hazieleweki yaani umepigwa katika mavazi au mapozi ya ajabuajabu, mara umebinua makalio, mara tumbo, mara mdomo, Haaaaa!
8. Kila unachofanya basi unakimbilia kupost.
Mfano kwenye Facebook yako au Instagram na nyinginezo hata ukienda haja basi lazima upost.

9. Ni mtu wa manenomaneno yu.
Yaani we kila unachokiona unakiongea na kuropokaropoka tu hauna breki, mwanamke gani?

10. Huna mawazo ya malengo endelevu.
Yaani we kwenye bichwa lako kumejaa umbea tu sijui leo Wema Sepetu kafanya nini? Sijui Kim, Rihanna, utazeeka!!!