Friday, October 12, 2018

KITABU CHA MAZOEZI YA KUONGEZA UREFU WA MWILI WAKO

watu wengi ambao ni wafupi hua wanakwazwa sana na maumbile ya kimo chao, wengi huathirika kiasaikolojia na kupewa majina mbalimbali,kuna sababu nyingi za kila mtu kupenda kua mrefu kama kujiamini mbele za watu, kupendeza kwenye nguo nyingi, ajira nyingine zinataka watu warefu kama ulinzi, jeshini na maonyesho ya mavazi au modelling na kadhalika...
watu wengi wana uwezo wa kuongeza urefu wa kimo chao kwa kutumia mazoezi fulani fulani ya mwili, mara nyingi urefu wa mifupa ya miguu na mapaja huacha kuongezeka mtu akifikisha miaka 20 mpaka 25 lakini urefu wa mgongo huweza kuongezeka mpaka miaka 40 na 50 kwani kuna ushahidi wa watu ambao wamefanikiwa kufanya hivyo.
sehemu zipi za mwili zinaweza kuongezeka urefu?
kama nilivyosema hapo juu, kuna sehemu kuna sehemu kuu mbili ambazo zinamfanya mtu aonekane mrefu na ndio hizo pia zinaweza kuongezwa urefu kama ifuatavyo.
miguu na mapaja; miguu na mapaja ina mifupa kitaalamu kama femur, tibia na fibula...hii ni mifupa ambayo ikiwa mirefu mtu anaonekana mrefu na ikiwa mfupi mtu anaonekana mfupi, urefu wa mifupa hii hua haupungui maisha yote ya binadamu na mara nyingi mifupa hii huacha kuongezeka urefu kwenye umri wa miaka 20 mpaka 25, hivyo kabla ya miaka 25 kuna mazoezi unaweza kufanya kurefusha mifupa hii lakini baada ya 25 haiwezekani tena.
                                                   
uti wa mgongo; uti wa mgongo ni sehemu ya pili ya mwili ambayo humfanya mtu aonekane mrefu au mfupi, eneo hili lina mifupa 33 ambayo imeungana kama pingili na kuacha nafasi katikati, hizi nafasi za katikati ndizo unaweza kuzifanyia mazoezi kuziongeza urefu kwa kuzivuta na kuonekana mrefu..kawaida umri unavyozidi kwenda pingili hizi zinazidi kubana kutokana na kusukumwa na kani ya msukumo au force of gravity ambayo inatusukuma chini na shughuli mbalimbali za kubeba vitu kichwani..hali hii humfanya mtu aliyekua mrefu wakati wa ujana kuendelea kupungua urefu umri unavyozidi kwenda isipokua yule ambaye anafanya mazoezi haya ndio anaweza asipungue.mtu mwenye umri wowote anaweza kufanya mazoezi ya kuongeza urefu wa pingili hizi.
                                                               

vitu gani vinafanya mtu awe mrefu au mfupi?
kuna sababu kuu mbili ambazo zimegawanyika kwenye vipengele mbalimbali
sababu za urithi[genetics]; 
urefu mara nyingi unafuata ukoo, japokua baba yako na mama yako kua wafupi haimaanishi na wewe lazima utakua mfupi, kama kuna ndugu wengine warefu kwenye ukoo unaweza kurithi urefu huo ukawa mrefu.
hakuna njia sahihi kabisa ya kujua utakua mrefu kiasi gani mpaka utakapofikia utu uzima lakini kuna jinsi unaweza kukadiria urefu wako kwa kuangalia urefu wa wazazi.
kanuni  iko hivi; urefu wa baba yako jumlisha urefu wa mama yako gawanya kwa mbili kisha ongeza 5 kama wewe mwanaume na punguza 5 kama wewe ni mwanamke.
mfano. baba yako ana urefu sentimita 160 na mama yako sentimita 160, ukijumlisha unapata 320 ukigawanya kwa mbili unapata 160...kama wewe ni msichana toa tano, unakadiriwa kua na urefu wa sentimita 155, na kama mvulana jumlisha tano unakadiriwa kufikisha 165.

sababu ambazo sio za urithi; hizi ni sababu ambazo zinaweza kumfanya mtu ambaye amezaliwa kwenye familia ya watu warefu awe mfupi ukubwani, mfano kukosa lishe ya kutosha kipindi cha utoto, kuugua sana utotoni, kuzaliwa na uzito mdogo sana, uvutaji wa sigara na pombe kwa mama mjamzito akiwa tumboni na kadhalika...

japokua mambo mengi sana yana amua mtu awe mrefu kiasi gani kipindi cha maisha yake lakini kuna mambo unaweza kufanya kuongeza urefu wako kidogo na kua mrefu kiasilia kama ifuatavyo..
pata usingizi wa kutosha; kama wewe ni kijana mdogo ambaye unataka kurefuka zaidi au ni mtu mzima kidogo na umeamua kuingia kwenye programu hii ya urefu basi hakikisha usiku unapata masaa yako nane ya kulala kwani mtu akilala homoni za ukuaji kitaalamu kama growth hormone hutengenezwa wa wingi sana.

kunywa maji ya kutosha; maji yanaufanya mwili uweze kufanya kazi zake za kutumia chakula kirahisi na kuondoa sumu zote mwilini, ni vizuri kunywa angalau glass nane za maji kwa siku, na hii itasaidia sana kwenye ukuaji wako.

kaa mbali na vitu vinavyozuia kuongezeka urefu; pombe na matumizi ya dawa mbalimbali huzuia ukuaji kwa vijana wengi ambao wako kwenye kipindi cha ukuaji, mfano baadhi ya dawa za pumu huweza kuchelewesha ukuaji, usinywe kahawa kwani itakunyima usingizi wa kutosha na kukufanya ushindwe kuongezeka urefu.
                                           
weka utaratibu wa kukaa na kutembea vizuri; watu wengi sana wana tabia ya kutembea wamepinda mgongo, hii ni kwasababu ya kukaa muda mrefu wakifanya kazi na kujikuta wamezoea hali hii ya kupinda mgongo...hakikisha ukiwa umekaa unanyooka na ukitembea unanyooka, siku ukizoea hali hii utashangaa kuona urefu kiasi gani ulikua umeuficha mgongoni.
                                                       

kula vizuri; achana na vyakula kama chipsi, soda, biskuti, chocolate na kadhalika kwani havina msaada kwenye ukuaji wako na jikite kwenye vyakula asilia vyenye virutubisho mbalimbali kama ifuatavyo
calcium; madini haya ni muhimu sana kwenye ukuaji wa mifupa kwani 99% ya mifupa imetengenezwa na madini haya, unaweza kuyapata kwenye maziwa, mboga za majani, soya, samaki na dagaa.
vitamin d; madini haya hufanya kazi bega kwa bega na mwili kuhakikisha madini ya calcium yanatumika na hupatikana kwenye uyoga,samaki, mayai, maziwa na unaweza kupata madini haya kwenye jua la asubuhi.
zinc; haya ni madini muhimu yanayopatikana kwenye mayai na maziwa.
                                                             

kua na ratiba nzuri ya kula; kula mara tatu kwa siku mchanganyiko wa vyakula mbalimbali vya asilia, lakini chakula cha usiku usile zaidi ya saa mbili usiku.

tumia virutubisho vya kuongeza urefu; kuna virutubisho mbalimbali vyenye madini muhimu ambayoa yanahusika moja kwa moja kuongeza urefu, tafiti zinaonyesha watu wengi hawapati madini ya kutosha kwemnye milo yao hivyo virutubisho hivi ni muhimu sana na vimesaidia watu wengi ambao wanataka kuongezeka urefu wa kimo,.(wasiliana nasi kama unavihitaji, kwasasa tunaagiza nje ya nchi)
                                               

upasuaji; nchi zilizoendelea kuna utaratibu wa kuvunja mifupa ya miguu na kuiongeza kwa upasuaji, utaratibu huu unaweza kufanikiwa kuongeza nchi 3 mpaka nne lakini kuna madhara ambayo yanaweza kutokea kwa kujaribu kufanya upasuaji huu, huku kwetu aina hizo za upasuaji hakuna.                                                

mazoezi ya kuongeza urefu; pamoja na vitu vyote ambavyo nimevitaja hapo juu, mazoezi ndio muhimu sana sana katika harakati za kuongeza urefu, sio mazoezi yote lakini kuna mazoezi muhimu ambayo yanalenga moja kwa moja kuongeza urefu wa mifupa yako na kukufanya uwe mrefu, kutokana na urefu na picha ambazo zinatumika kuonyesha mazoezi hayo kua ndefu sana nimeamua kuandika kitabu cha mazoezi makuu ya kuongeza urefu wa binadamu baada ya kufanyia majairibio njia hizo na kugundua kwamba mazoezi hayo yanafaa iwapo yakichanganywa pamoja na virutubisho na mambo niliyoyasema kwenye makala hiii.
kulingana na ukubwa wa kazi uliofanyika kwenye tafiti hizi na maandalizi ya makala hizi na kitabu, kitabu hichi kitauzwa kwa gharama ya shilingi 20000[elfu ishirini tu] za kitanzania na kitakua kwa mfumo wa soft copy yaani kitatumwa kwa email au watsapp kwa ambao watakua tayari kukitumia ili wafanikiwe kuongeza urefu.
kuongeza urefu kunataka juhudi, bidii na kutokata tamaa...kama huwezi kupambana basi usipoteze fedha zako kununua kitabu hiki.

je kuna watu ambao walifanikiwa kwa mazoezi haya?
ndio watu maarufu kabisa duniani ambao zamani walikua wafupi au walikua warefu wa kawaida baadae walifanya mazoezi haya na kufanikiwa kuwa warefu, wapo naowafahamu binafsi yaani marafiki zangu, mimi pia niliwahi kuongezeka urefu kwa mazoezi haya, watu niliosoma nao shule ya msingi na sekondari wanakumbuka ufupi wangu, ila ntazungumzia wale maarufu ambao wanafahamika dunia nzima hii imewajengea heshima na kuwaongezea kipato kama ifuatavyo..
christiano ronaldo
akiwa na umri wa miaka 18 mchezaji huyu maarufu ambaye kwa sasa anacheza soka ka kulipwa huko ulaya katika timiu ya real madrid alikua na urefu wa futi tano na nchi kumi lakini alipofikisha miaka 25 alikua na urefu wa futi sita na nchi moja kwa mazoezi hayhaya  na njia hizihiz nayozungumzia hapa.

 schwarzeniger;
huyu ni moja ya watu maarufu sana ambaye aliwahi kujihusisha na ubebaji wa vitu vizito, uigizaji wa filamu na baadae kua gavana wa jimbo la calfornia nchini marekani. yeye aliongezeka kutoka futi sita mpaka futi sita na nchi mbili.
                                                       

david robinson;
huyu alikua anapenda sana kucheza mpira wa kikapu kama basketball lakini kutokana na ufupi wake hakuweza kuruhusiwa kufanya hivyo na baadae alikata tamaa, lakini kwa mazoezi hayahaya alitoka kwenye urefu wa tano na nchi tisa mpka futi saba na nchi moja, baadae alichezea ligi kubwa                                                    

kabisa duniani ya nba na kua kati ya watu wenye mafanikioa makubwa kwenye ligi hiyo.

andy murray; huyu ni mcheza tennis ambaye hapo mwanzo alikua na urefu wa futi sita na nchi moja lakini hivi karibuni amefanikiwa kufanya mazoezi na kuongezeka mpaka futi sita na nchi tatu.
                                                               

le jingy; huyu ni muogeleaji maarufu ambaye aliongezeka kutoka futi tano na nchi saba mpaka futi sita na nchi moja kwa kufanya mazoezi hayo.
                                           

dennis rodman; akiwa na urefu wa nchi 5 na futi nane alikataliwa kwenye timu ya basketball ya shuleni kwao na kujiingiza kwenye mazoezi haya, ambayo baadae yalimpa urefu wa futi sita na nchi nane na kufanikiwa sana kwenye mchezo huu.