Tuesday, April 10, 2018

Kwanini Wanawake Hudanganya Juu Ya Idadi Ya Wanaume Walio Lala Nao ?

Wanawake wengi wanadanganya idadi ya wanaume ambao wamesha lala nao. Kwasuala hili wamekuwa wanadanganya ili ku ficha kuwa sio wazuri kwenye mahusiano au ni namna gani amekuwa akishidwa kufikisha ahadi za mahusiano na kuachika au kuacha mahusiano yaliyo pita. Wanawake wengi wanakuwa na wasiwasi juu ya uwazi wao juu ya idadi ya wavulana walio nao au mahusiano yao wavulana watawadhani kuwa sio wakamilifu kwenye mahusiano napia sio wazuri kwenye mahaba kitandani. Pia wanahofu baadhi ya wanaume watawaona kuwa malaya au hawatulii kwenye mahusiano, kabla hujamsababisha mwanamke kwenda kwenye huo uongo wake, kuna vipengele muhimu kuvijua ili uweze kufika wakati wa kumuuliza hayo.

Wakati muafaka wa kumuuliza msichana juu ya mahusiano yake yaliyopita.

Kama unataka kumuuliza mwanake uliyempata juu ya mahusiano yaliyo pita au wangapi amelala nao kitandani inatakiwa kuwa na muda sahihi. Huwezi kuuliza swali hilo wakati mnatoka kwa mara ya kwanza au wakati mpo kwenye mapumziko kama hotelini au bar. Hii itakuwa umeharibu kila namna ya wewe kupata ukweli. Kila mwanamke atakuwa na aibu au woga kwa mwanaume anaye uliza swali zito kama hili mapema hata mahusiano hayajaanza kuwa makini. Pale mvulana anapofanya hivyo basi mwanamke lazima atadanganya na kuficha. Ni rahisi kuuliza swali hilo baada ya kuwa mmezoeana na kuwa mnatoka out mara kadhaa. Pale mwanamke atakapoona upo naye na unajali kujua basi atakuwa radhi kukwambia ukweli.

Japokuwa kwa wavulana ni rahisi kwao kutaja kuwa nilisha lala na wanawake kumi au zaidi. Pale mwanamke anapo taja hivyo anadharaulika na ndio maana haishangazi kwa wanawake kudanganya.

Je wavulana wanayo haki kuuliza?

Labda kama msichana ambaye upo naye unajua alikuwa malaya wa kujiuza au mcheza filamu za ngono basi hamna haja ya wewe kuuliza maana itakuwa haikuhusu. Kwamaana jambo ambalo haulijui ukweli wake halitakuumiza moyo wako. Kwakuongezea nikwamba kila msichana/mwanamke hudanganya juu ya idadi ya wavulana alio kuwa nao au alio wahi kulala nao. Na hili halitasababisha kubadilisha mahusiano yenu mnayo taka kuyaanza.

Kwanini wavulana hawapati ukweli kwenye suala hili!

Kuna ngono wanawake walizo zifanya ambazo hawataki kuzizungumzia kamwe. Kwasuala hilo nikama kunyanyapaa. Kwa mfano, Alijikuta amebakwa au amefanya ngono bila kupenda wakati akiwa high school au chuo. Kwahiyo hutakuja kujua kuhusiana na jamaa aliye lala naye wakati akiwa amelewa na kufanya naye ngono. Kwa wanawake wengi nivigumu kujadili juu ya hilo.

Itakuwa ni vyema kwa wavulana kumkubali mwanamke bila kutaka kujua yaliyo pita kwake. Wanawake wanadanganya, lakini nia ni kutunza utu wake na heshima ya mwanamke. Hawataki wavulana wawachukulie kama mtumwa wa mapenzi au malaya kutokana na aliyo yapitia. Wavulana wengi hudanganya juu ya emotional kwenye msichana anaye mvulia au tamaa za mwili kwa mwingine. Wanawake nao hudanganya juu ya wavulana walio ngonoka nao. Nijambo la kuficha kwa mvulana kudanganya hisia zake za kweli na msichana kudanganya ili asijulikane marangapi kalalwa kitandani.