Saturday, April 7, 2018

Aina 12 za wanaume ambao binti hata awe mjanja vipi atakutana nao katika maisha yake

MR. THUG LIFE 
Faida zake 
Hukufurahisha na ya kukusisimua
Hufanya ucheke
Anakua pembeni yako kwa kila jambo na atakupigania na kukulinda 
Hasara 
Mara nyingi wanatabia za kunywa pombe na kuvuta sana sigara
Kila mra hakosi drama za kukushangaza
Atakuwa katika hali hiyo ya ukorofi milele 
Kushikwa na kuwekwa jela ni kawaida yao kutokana na drama zao 
MR. KWA SASA SINA MSICHANA 
Faida zake 
Atakuchukua na kukutoa out kila mara
Atakutambulisha kwa marafiki zake wote
Atakuwa ni mtu wa kukupa pongezi wakati wote 
Hasara 
Anamchumba ambaye wako naye kwa muda mrefu
Hawezi kukuambia kuwa ana mchumba
Baada ya kuteka moyo wako nawe umedata ndio atakuambia kuwa ana mpenzi 
MR. MAARUFU 
Faida zake 
Atakupa fedha nyingi na hakuna kukulizwa maswali
Ana style nyingi za jinsi anavyoendesha maisha yake
Atakuonyesha baadhi ya mambo mazuri katika maisha yako 
Hasara 
Kamwe usije jaribu kuishika simu yake
Anamaamuzi ya kutokukushirikisha, anaweza kuja nyumbani kwako wakati wowote bila kutoa taarifa
Anapenda kuwa karibu na marafiki zake zaidi kuliko wewe. 
MR. MISHEMISHE A.K.A JEMBE 
Faida zake 
Anaweza kukupa mialiko wewe na marafikio zako katika minuso mbalimbali na kumbi nyingi za
Unaweza kuwa na heshima na kila uongeacho na kuchochea mazungumzo pia
Anavaaa nguo za gharama 
Hasara 
Huwezi kujua kama yeye ni shoga au lah kwani hana kazi, muda wote yupo kwake na huoni dalili za kuhangaika lakini ana maisha mema na pombe kila siku
Hujifanya anakuwa mkali ukijaribu kumwelezea juu ya mpango wa mahusiano yenu kwenda mbele
Ukiwa bado kwenye mstari wa kupata tiketi uingie kwenye pati, au mnuso unaweza kushuhudia drama pale mlangoni na kisha mkaruhusiwa kuingia
Ana rundo la picha za yeye na celebrities kibao lakini hawajuani na mmpoja kati ya hao mastaa 
MR. MSOMI 
Faida zake 
Muda wote yupo smart
Anakujali na kuhakikisha unajisikia vyema 
c.Ana kazi nzuri sana 
hasara 
Mambo yake yanaboa sana kwani muda mwingi anahangaika na mambo ya kazi
Hata kwa bed ni mvivu sana kwana anakuwas kachoka na majukumu
Hayuko smart sana na mambo ya mtaani kama kukutoa out kwani anakuwa busy
Daima ni mtu wa kukuliza lini tutaonana tena 
MR. GETO 
Faida zake 
Hukufanya ucheke
Anavutia kuwa naye karibu
Ana hasira za haraka, lakini kwa ujumla ni mtu poa
Atasema yeye anataka uhusiano wa kweli 
Hasara 
Ana watoto 3 au zaidi kwa mama tofauti
Anataka kukutumia apate chakula, fedha za matumizi na sio upendo
Na kila ukimwambia ukweli juu ya mambo yake anakataa au kuwa mkali
Kama ukikaa naer anaweza rudi hata saa tisa usiku na kujitetea alikuwa na marafiki 
MR. RASTA 
Faida zake 
Atakufundisha mambo mengi ya upendo na amani 
Yeye ni mwanaharakati au mwanamapinduzi
Atakupa maneno na falsafa zenye kukupa msukumo wa amani na ni maneno ya kihalisa yenye hisia
Anataka mke na familia 
Hasara 
Atakupiga chini akipata binti wa kizungu
Ana hela za kufanyia starehe ila hana kazi maalumu
Haimiliki suti nzuri, siku zote amevaa kombati au jinsi na kutokwa na jasho
Mwishoni utagundua kuwa alikuwa anakuigizia 
MR. FUTURE 
Faida zake 
Atakutambulisha kwa mama yake
Ana kazi na atakuwa mtu wa kujirusha na wewe
Atakupa fedha za mahitaji yako kama unahitaji
Wakati mwingine huenda kanisani Jumapili 
Hasara 
Wakati mwingine naye anataka kuwa mtu wa kuishi free
Ni mtu wa kuvaa mikufu na saa fake
Kuna wakati yeye yuko busy na kufuatilia michezo aipendayo na kukusahau wewe kama upo
Baada ya kuachana ndio utagundua alikuwa ana mabinti kibao. 
MR. KICHECHE 
Faida zake 
Atakuambia ukweli – kwamba wewe sio mmoja tu kwake
Yeye atakwambia kwamba umembadilisha na yuko tayari kutulia na wewe
Anakaa kwake ana usafiri na atakuomba uhamie pale make wote 
Hasara 
Hawezi kukutambulisha kuwa wewe ni mpenzi wake mkiwa sehemu hasa akiona kuna wanawake
Kwa ujumla yeye ni mzushi wa kila afanyacho
Anatarajia wewe kuamini uongo wake wote kwa sababu tu alikuambia ukweli kuhusu wanawake wengine alipkuwa nao
Baada ya kumdaka uongo wake atajitetea alishakuambia kuwa alikuwa kicheche 
MR.NINA KAZI NZURI 
Faida zake 
Bila shaka ana kazi
Hana tabia nyingi mbaya sana 
c.Atachukua wajibu wa kukuhudumia wewe wakati wewe ni mgonjwa 
Atakwambia kwamba yeye ana upendo wa dhati na wewe 
Hasara 
Utadumu naye katika uhusiano wa miaka 2 au zaidi na kisha unakuja kugundua ni mvivu, mpuuzi na bedui ambaye anataka wewe kufanya kazi zote za mke lakini si kukupa pete.
Atamaliza kwa kukuambia anakupenda ila wewe sio chaguo lake
Baada ya kukuacha miezi mitatu baadae anafunga ndoa 
MR. RAFIKI WA UHAKIKA 
Faida zake 
Yeye ni rafiki yako bora, uamweleza kila kitu kinachokusibu na mnakwenda pamoja vizuri sana
Anatoa ushauri kwa wakati unapopatwa na matatizo
Ni mwanaume wa kweli 
mwelewa na anakujali na ni mcheshi wa kupindukia 
Hasara 
Manishia kujirusha na mwishowe unakuja kugundua hana lolote yeye anataka sex basi.
Hapo unahitaji kupata mpenzi mpya kwani yeye hana mpango wa maisha na wewe 
MR. MWANAUME SAHIHI 
Faida zake 
Yeye anampenda Mungu na anachukua uhusiano wake na Mungu kwa umakini
Yeye ni mwelewa, ana kipaji na uwezo wa kukuchukua wewe kiakili na kihisia
Naye atakupenda hata wakati wewe haupendeki
Yeye ana ujuzi wa kufanya kazi kwa ustadi na anapendwa !
Anakubali makosa yake na inajitahidi kuwa mtu bora
Anaelewa uhusiano unajengwa kwa 200% . Yeye100% na wewe 100%
Yeye hana kundi la watoto wa mama, yeye ni nadhifu zaidi na anakitambua.
Yeye ni rafiki wa bora wa kweli na kila kitu unachotaka kwa mwanaume yeye anacho
Alikuwa mzuri ulivyokutana naye ila baada ya kukaa naye unagundua anazidi kuwa nadhifi zaidi
Anaweza kupangilia mavazi – anajua tofauti kati ya mavazi rasmi , ya kawaida, ya kitaaluma, ya biashara
Yeye anampenda mama yake na kuheshimu wanawake 
Hasara 
Hujawahi kutana naye na kama yupo basi ana mke au mchumba .
Yeye hataki uhusiano wowote kwa sasa

Umeshamsikia sana mtu wa aina hii lakini kamwe hujakutana naye na lazaidi umeshakutana na aina hizo hapo juu za wanaume na wakakuchezea vilivyo