Saturday, January 13, 2018

Je una skin Tags, Umejaribu njia hizi kuondoa?

Skin Tags ni vile vimaoteo vya ngozi vilaini vyeusi au brown ambavyo huota sehemu mbalimbali za mwili, kama vinavyoonekana hapa

Kwanini unapata Skin tags?
Inasemekana mambo yafuatayo hupelekea kupata skin tags

1. kurithi
2.Baadhi wanahusisha skin tags na maradhi ya kisukari
3.Umri mkubwa
4. Msuguano wa ngozi, Mfano shingoni kutokana na uvaaji mikufu
5. Mabadiliko ya vichocheo (hormones)
6. Matumizi ya madawa yenye vichocheo ( steroids) bila kufuata ushauri wa daktari

Njia za kuweza kuondoa

1. Kutumia Tea Tree Oil

Mafuta haya yanasemekana kuwa na uwezo wa kutatua matatizo mbalimbali ya ngozi pia hutumika katika vipodozi vingi. Yanafanya kazi kwenye virusi, bakteria na fangasi pia
Related image
Matumizi:
  1. Chukua pamba kidogo loweka kwenye maji
  2. Chukua matone kama matatu mimina kwenye pamba iliyoloa.
  3. Paka kwa kuzungusha kwenye sehemu husika
  4. Endelea kufanya hivi kila siku kwa siku 10 huku ukiangalia matokeo

2. Tumia Oregano Oil

Haya mafuta yanatajwa kuwa na uwezo wa kuua bakteria, kuzuia hali ya mzio (anti inflammatory properties) kwenye ngozi, kuzuia kuchakaa au kuzeeka kwa seli za ngozi pia yanatajwa kuwa na uwezo wa kutatua tatizo hili kwa haraka.
Image result for oregano oil
Matumizi: 
  1. chukua matone matatu ya oregano na changanya na mafuta ya nazi matone matano
  2. Paka mchanganyiko wa mafuta haya sehemu iliyoathirika
  3. Usitumie karibu na macho tafadhali

3.Tumia Castor Oil ( mafuta ya nyonyo) na Baking Soda

Mafuta ya nyonyo yanatumika katika kuondoa madoa na vitu visivyotakiwa katika ngozi na kutoacha alama. Yanatajwa kuwa na virutubisho kwa ajili ya afya ya ngozi.

Matumizi
  1. Chukua mafuta ya nyonyo kisha weka baking soda kutengeneza uji mzito (paste)
  2. Paka sehemu yanye skin tag kisha funga na bandage
  3. Unaweza kuweka mafuta ya ndimu au limao kupata matokeo mazuri zaidi.
  4. Fanya hivi kwa mwezi au mpaka pale kitakapopotea

4. Apple Cider Vinegar

Apple cider vinegar imetajwa kwamba inaweza kusaidia kwa kuharibu "tissue" ya skin tag, hii inafaa kwa vile vilivyoota shingoni.

Matumizi
  1. chukuapamba chovya kwenye siki ya matofaa ( Apple cider vinegar)
  2. paka pale kilipoota kwa kusugu dakika 5
  3. Fanya kwa mwezi mmoja huku ukiangalia mabadiliko

5. Ganda la ndizi

 

Matumizi:
  1. weka kipande cha ganda la ndizi sehemu iliyoathirika hlf funga na bandage/plasta
  2. Hakikisha kwa ndani ndio kunagusana na skin tag
  3. lala na kipande cha ndizi mpk asubuhi
  4. Fanya hivi mpk kitakapopotea

6. Juice ya kitunguu

 

Inasemekana kitunguu kina uwezo wa kusinyaisha (shrinking) hizi skin tags pia kina asili ya asidi.

Matumizi
  1. chukua vipande vidogo vya kitunguu
  2. Loweka vipande vya kitunguu katika maji
  3. Chukua maji yaji ya kitunguu na chumvi kisha paka kwenye sehemu iliyoathirika
  4. Lala na mchanganyiko huo mpk asubuhi kisha osha na maji vuguvugu asubuhi
  5. Endelea kufanya hivi kwa wiki moja

7. Maji ya limao

Maji ya limao yana asidi pia yana uwezo wa kuua baadhi ya vimelea, inasemekana yana uwezo wa kuvimaliza hivi vijipele.
 
Matumizi
  1. Tumia pamba kupaka maji ya limao sehemu iliyoathirika
  2. baki na maji ya limao mpaka yakaukie hapo
  3. Fanya hivi kwa siku kadhaa hadi wiki huku ukiangalia mabadiliko

8.  Aloe Vera Gel (ute wa mshubiri)

Aloevera (shubiri) inasifika katika kutatua matatizo mbalimbali ya ngozi pia inasemekana inaweza kuondoa skin tags. 
 
Matumizi
Paka ute wa aloevera kwenye sehemu iliyoathirika. 

9. Kitunguu swaumu

Kitunguu swaumu kinasikifika kwa uwezo wa kutibu matatizo mbalimbali yanayoletwa na fangasi hata bacteria inasemekana kina uwezo wa kukausha skin tags kwa kuwa kuna vichocheo (enzymes).

Matumizi
  1. twanga kitunguu saumu upate uji mzito
  2. paka moja kwa moja sehemu iliyoathirika kisha funga na plasta
  3. Unaweza kufanya mara mbili kwa wiki

10. Tangawizi

Tangawizi ina sifa zinazofanana na kitunguu saumu, inaweza kutumika kupambana na seli za skin tags.

Matumizi
  1. Twanga tangawizi kama ulivyofanya kwa kitunguu saumu.
  2. unaweza kukata vipande vidogovidogo
  3. Tumia ndani ya wiki mbili utaona mabadiliko

11. Vitamini E

Inasemekana mafuta yenye vitamini E yana uwezo wa kuondoa skin tags.
  1. Paka mafuta ya vitamin E sehemu iliyoathirika.
  2. Unahitaji kupaka kwa wiki moja hadi mbili
  3. Unaweza kupata matokeo mazuri ukichanganya kitunguu saumu na mafute ya vitamini E

 

12. Nanasi

 

Nanasi linasikifika kuweza kupausha muonekano wa skin tags na kisha kufanya zipotee.

Matumizi
  1. Paka maji ya nanasi sehemu iliyoathirika
  2. Paka kwa siku 8 hadi 10, usifute au kuosha baada ya kupaka

13. Rangi ya kucha

 

Inasemekana rangi ya kucha ikipakwa sehemu iliyoathirika kwa muda skin tag inapotea.

 Nunua rangi ya kucha nzuri, tumia uliyonayo kupaka sehemu iliyoathirika
  1. Paka mara 2 hadi 3 kwa siku
  2. Baada ya siku chache utagundua skin tags zinakauka na kuondoka zenyewe
  3. Iwapo skin tags zipo sehemu za siri au karibu na jicho epuka kutumia rangi za kucha hapo.

14. Kufunga uzi

Hii mbinu ni ya siku nyingi ambapo unafunga mzizi na kukaza mpaka kinatoka, hapa unaweza kutumia barafu kuweka ganzi ili usisikie maumivu.

15. Nail clipper au tuiser

Kwa vifaa hivi unaweza kukata kuanzia kwenye mzizi na kukiondoa mahali pake, Angalia ambavyo ngozi yako inareact kwa kuondoa kimoja kwanza.

Hizo ndio njia zinazozungumziwa, kazi kuzijaribu tu.
much love